Naukumbuka msimu ule wa 2007/2008 wakati manchester
united ikiwa kwenye ubora wake, wakati huo Manchester united ikiwa chini ya sir
Alex Ferguson iliweza kuzoa mataji maatu lile la ligi kuu uingereza, kombe la
FA na klabu bingwa Ulaya, wingi wa mashabiki wa upinzani kuipinga united katika
maeneo ya maeneo ya kuoneshea mpira hii ilidhihirisha ni jinsi gani man united
ilikuwa bora.
Huo ulikuwa wakati ambao Christian Ronaldo aliweza
kutwaa tuzo ya mchezaji bora ulaya na mchezaji bora wa dunia nyuma ya Lionel
Messi ambaye ndiye alikuwa ameanza kuwa kwenye ubora wake, Ronaldo alijiunga na
Real Madrid akiwa bora na bila shaka aliweza kukubali kujiunga na Real Madrid
kwa kuwa ilikuwa bora.
Tangu kustaafu kwa mkongwe sir Alex Ferguson bado
united imeshindwa kurejea kwenye ubora wake, David Moyes ambaye ndiye aliyekuwa
chaguo la sir Alex Ferguson aliweza kudumu kwa miezi nane na kuinyima timu hiyo
fursa ya kushiriki michuano ya mabingwa ulaya na baadae alikabidhiwa kocha
Louis Van Gaal ambaye naye hajairejesha timu hiyo kwenye ubora wake.
Louis Van Gaal amekuja na wazo jipya la kumsajili
nyota wa Brazil Neymar Jr ambaye anafanya vizuri kwenye timu ya Barcelona
akishirikiana vizuri na Lionel Messi pamoja na Luis Suarez ambaye anatisha kwa
kutikisa nyavu kwa wapinzani wake, Neymar amekuwa kwenye wakati mzuri katika
timu ya Barcelona na aliweza kuingia kwenye
tatu bora ya kinyang’anyiro cha kutafuta mchezaji bora wa dunia.
Pamoja na tetesi kuwa Manchester united imetengenga
euro 140 milioni za kumsajili nyota huyo binafsi naona ni ndoto za mchana
ambazo hazina mafanikio. Kwa sasa timu za Hispania zimekuwa bora ilikinganishwa
na zile za Uingereza ukianza na Barcelona na Real Madrid ambao ni miamba wa La
liga, Atletico Madrid pia chini ya Simeon imekuwa kwenye wakati mzuri bila
kuisahau Sevilla ambao wanatisha kwenye michuano ya europa.
Manchester united ilishindwa kuvuka kuelekea katika
hatua ya 16 bora katika michuano mabingwa ulaya baada ya kukubali kipigo kutoka kwa Wolfsburg na
hatimaye kutupwa katika michuano ya europa. wachezaji wengi bora lazima wafanye
vizuri kwenye ligi zao, na mashindano mengine, kama ilivyokuwa kwa Lionel Messi
ambaye alikusanya mataji yote muhimu na kuibuka bora msimu huu.
Kama Neymar anataka kuwa bora kama Messi ni wazi
kuwa united watakuwa wanatwanga maji kwenye kinu kwa kutoa ofa hiyo, jibu liko
wazi kwa sasa huwezi kuwa bora duniani ukiwa na Machester united, ingawa
Manchester united ni timu kubwa duniani lakini inahitaji kurudi kwenye ubora
wake kwanza ndipo ianze kuhangaika na wakina Neymar ambao wanaweza kuibuka bora
kama timu hiyo itarudi kwenye ule ubora wake.
Real Madrid, Barcelona na Bayern Munich zinaweza
kusajili nyota wa kubwa na kuipiku Manchester united kwasababu zipo kwenye
ubora na ndizo zinazofanya vizuri katika
michuano ya ndani na kabu bingwa ulaya hivyo kuna njia ya mafanikio kwa
wachezaji bora wa timu hizo kuliko ilivyo kwa united, wakati huu ambao Edwood
Ward na Louis Van Gaal wapo kwenye harakati za kuikomboa timu hiyo.
Ikumbukwe Barcelona ndiyo timu inayoongoza kutoa
kutoa wachezaji bora duniani, hayo ni matumaini tosha kwa Neymar ambaye ana
imani siku moja atakua bora ilivyokuwa kwa lionel kulingana na kiwango chake
kuwa bora wakati wote. Ikumbukwe Ronaldinho Gaucho alikuwa bora wakati lionel
messi anachipukia, Neymar 23, yuko nyuma kwa miaka mitano dhidi ya Messi ambaye
umri wake ni miaka 28, matumaini yake ni kuwa mtawala wa pale Catalunya baada
ya kuondoka kwa ufalme wa Messi na wala si suarez ambaye ana umri sawa na
lionel Messi.
Ndiyo maana nilinza kwa kuikumbuka Manchester united
ambayo ilimuinua Ronaldo kuwa bora wakati ule wa Ferguson bila shaka alistahili
kuchukua tuzo akiwa kwenye timu bora ambayo ilikuwa inaundwa na wachezaji bora.
Wakati ule Ronaldo anavunja rekodi ya usajili kwa dau la pauni million 80 bila
shaka halikuwa dau pekee lililoweza kumshawishi kutua Santiago Bernabeu bali ni
sifa na ubora wa ambao timu ya Madrid ilikuwa nayo na ndiyo maana akiwa na timu
hiyo ameweza kuweka na kuvunja rekodi mbalimbali na kuongeza tuzo mbili za kuwa
bora duniani.
Kama hali haiko shwari pale Old Trafford ni vigumu
Neymar kutua Man united, pamoja na kiasi kikubwa walichotenga hakitaweza
kumfanya Neymar kuwa bora duniani. Diego Simeon ambaye ni kocha wa Atletico
Madrid aliwahi kunukuliwa akimwambia aliyekuwa kocha real Madrid Carlo
Ancelloti hatomfunga tena kama amemwachia Di Maria atimke kwenda united.
Diego Simeon anakumbuka vema kazi ya Di Maria ambayo
ilimpokonya taji la klabu bingwa mdomoni, licha ya kutua kwa mashetani hao
Angel Di Maria akiwa kwenye kiwango bora alishindwa kufanya vizuri akiwa Luis
Van Gaal pale Man united hilo ni tatizo lingine ambalo linaweza kumtisha Neymar
ambaye ana matarajio ya kuwa nyota zaidi katika soka, ambaye anafikiria kuwa
mwenye mafanikio kama Lionel Messi aingie kwenye kumbukumbu ya vitabu vya
wachezaji nguli wa soka duniani
Binafsi naziona euro 140 milioni haziwezi kufanya kazi
ya kumleta Neymar pale old trafford labda ubora ule wa Manchester united katika
ule msimu wa 2007/08 ambao ulimpa tuzo Christian Ronaldo kwa mara ya kwanza
ndiyo unaoweza kumleta Neymar Man united kwa sababu atakuwa na imani ya kuwa
bora akiwa na timu iliyo bora na heshima ile ambayo ilijiwekea dunani.

Comments
Post a Comment