Mashabiki waisimamisha mechi ya Stand united na Mwadui fc






Mashabiki wa timu ya Stand united walileta vurugu na kupelekea kusimama kwa mchezo wa kombe la FA uliochezwa jana dhidi ya mwadui fc katika uwanja wa Kambarage mkoani shinyanga.

Vurugu hizo zilitokea dakika ya 88 ya mchezo baada ya mashabiki hao kutoridhishwa na maamuzi ya mwamuzi wa mchezo huo ambaye alionekana kuipendelea timu ya Mwadui fc baada ya kutoa penati katika dakika ya 65 na kukataa bao la kusawazisha kwa Stand united dakika 88 kutokana na Elias Maguli kuunawa mpira kabla ya kutoa pasi ya goli na kupelekea mchezo huo kusimama kwa takribani dakika saba.

Kocha wa stand stand united Patrick Liewing  alijihami kwa kukinga kichwa chake na kiti kutokana na kurushwa kwa mawe na chupa za maji uwanjani kutoka kwa mashabiki waliokuwa wamejawa na hasira baada ya kutoridhishwa na mwenendo wa mchezo.


Mchezo huo uliendelea baada ya jeshi la polisi kuimarisha ulinzi na usalama na kurejea kwa amani ya mchezo, hadi mwisho wa mtanange huo Stand united ilishindwa kusawazisha bao pekee lililowekwa nyavuni kwa mkwaju wa penati na Jeryson Tegete na hivyo kuyaaga rasmi mshindano hayo. 

Comments