Naukumbuka ubora wa Nemanja, Naukumbuka na ule ubora
wa Branslav Ivanovic ambao wote walitamba na kufanya vizuri wakiwa katika ligi
ya Uingereza licha ya kucheza timu tofauti lakini bila shaka Wasebia hao
walikua gumzo kutokana na kuwa wagumu kupitika katika safu ya ulinzi, namkumbuka Rio Ferdinand alivyoishi maisha rahisi pale
Manchester united chini ya ulinzi mkali wa Nemanja Vidic, licha ya kusajiliwa
kama mlinzi wa kati katika timu ya Chelsea Branslav Ivanovic aliweza kuwa bora
kwa kucheza kama mlinzi wa kulia na beki wa kati pale inapobidi kumsaidia John
Terry au Ricardo Carvalho, na hadi sasa bado anaishikilia namba pale Stamford
Bridge.
Uzuri wa mabeki hao ulizifanya timu za Uingereza kugeuza macho na kuelekea ulaya mashariki
kunako nchi ya Serbia ili kupata walinzi bora ambapo usajili wa mabeki na
viungo imara wa kukaba kwa wachezaji kama Nemannja Matic ulifatia.
Naliona hili katika klabu za Tanzania hasa Simba na
Yanga, hapa naizungumzia ardhi ya Robert Mugabe ambayo imetuletea mshambuliaji
bora katika klabu yanga Donald Ngoma,
kiungo bora Thabani Kamusoko na Yule aliyesajiliwa na simba Justice Majabvi.
Wote hawa wajihakikishia namba za kudumu katika timu zao kutokana na kufanya
vizuri.
Nikimwangalia Donald Ngoma natamani angekuwa
mtanzania ili stars yetu ifike mbali kwa kuwa na wachezaji bora ambao wanaweza
kubeba majukumu uwanjani, licha ya kucheza nyuma ya mshambuliaji Amis Tambwe
lakini bado Ngoma anazidi kuwa bora, huyu jamaa ana uwezo wa kuendesha timu,
kufunga na kutoa pasi za magoli kwa mshambuliaji wake, ni msumbufu na huwaweka
walinzi katika wakati mgumu muda wote awapo uwanjani.
Nakumbuka katika ya kombe la mapinduzi baada ya
Ngoma kufanyiwa mabadiliko dhidi ya URA ya Uganda, URA ilipata matumaini mapya
ya kushambulia kwa kuwa waliamini ni aliyetoka alikuwa tishio kutokana na uwezo
wake wa hali ya juu na kasi aliyonayo uwanjani hivyo hawakuwa na hofu
iliyowafanya wasipandishe mashambulizi. Mpaka
sasa Donald Ngoma ameifungia yanga magoli 9 katika mechi 15 za VPL alizocheza.
Namwangalia
kiungo huyu mtulivu aliyewafanya makocha na viongozi wa Yanga wamfungie Kiungo
Haruna Niyonzima maarufu kama Fabrigas
bila hofu licha ya umahiri wake mkubwa wa kupiga pasi uwanjani lakini kiungo
Thabani Kamusoko alidhihirisha jeuri ya timu hiyo kwamba wanaweza kufanya
vizuri bila Haruna Niyonzima ambaye hivi karibuni aliomba msamaha kwa timu yake.
Thabani Kamusoko ni kiungo bora ambaye anaweza
kuituliza timu, kupiga pasi, kuongoza mashambulizi na uwezo wa kufunga magoli,
anapenda kucheza mpira amekuwa shida kwa viungo wa timu za upinzani na
kudhirisha kuwa yeye ni mkali ameiwezesha timu yake kukusanya pointi 39 ikiwa
kileleni mwa ligi bila uwepo wa kiungo tegemezi Haruna Niyonzima.
Ukirejea katika ule mtaa wa msimbazi bila shaka
utamkuta Justice Majabvi ambaye alisajiliwa kutoka uko kwenye ardhi walikotoka
wakina Dornald ngoma na Thabani Ngoma, tofauti ni timu walizocheza. Kiungo uyo
ana uwezo mkubwa wa kukaba na mtulivu katika kucheza mpira katikati, amekuwa
muhimu kwa kikosi cha msimbazi, Justice
Majabvi ana uwezo wa kucheza kama kiungo
mkabaji na beki wa kati na alicheza mara kadhaa kwenye nafasi hiyo akiwa na
timu yake ya simba.
Naipenda ile timu yangu ya Ukraine maarufu kama
Shakhtar Donetsk ambayo imekuwa ikisajali wachezaji wengi kutoka nchini Brazil
ambao wamekuwa msaada mkubwa kwenye ligi yao ya nyumbani na kufanya vizuri
katika mashindano ya klabu bingwa na yale ya Europa. Shakhtar wamegundua
wachezaji hao wana msaada mkubwa kwao na ndiyo maana Brazil imekuwa shimo lao
kubwa la usajili kuliko wachezaji wa nchi za ulaya, ambapo wameweza kuwauza
wachezaji ambao ni nyota Luiz Adriano ambaye sasa ni mashambbuliaji wa Ac Milan
alimfukuza Christian Ronaldo kwa magoli kwenye michuano ya klabu bingwa ulaya
msimu uliopita na Willian da Silva ambaye anang’aa na Chelsea.
Nina mashaka pengine macho ya usajili ya timu zetu
za Simba na Yanga hapa Tanzania kuelekea katika ardhi ya Robert Mugabe kwa
ajili ya kusaka nyota ambao wataleta ushindani kitaifa na kimataifa , kama
wanafanya vizuri kama tunavyoona kutoka kwa kina Ngoma, Kamusoko na Majabvi
itakuwa rahisi kwa timu zetu kusajili kutoka Zimbabwe kama ilivyo kwa Shakhtar
Donetsk kutoka Brazil. Pengine tutahama Kenya na Uganda na macho ya usajili
yatalenga zaidi katika nchi ya Zimbwabwe ambayo nyota wake watatu wameweza
kuitangaza nchi yao hapa Tanzania.

Comments
Post a Comment