Eric Bailly afanyiwa vipimo Man united


Timu ya Manchester united imekamilisha zoezi la vipimo kwa beki wa kati wa timu ya Villareal Eric Bailly ambaye yupo mbioni kutua Old Trafford.

Bailly 22, anafukuziwa na timu mbalimbali ikiwemo Manchester city, Barcelona na Paris Saint-Germain lakini hadi sasa Manchester united inaongoza kwenye mbio za kumsajili Beki huyo.

Manchester united huenda ikamwaga mzigo wa euro 31 milioni ili kumaliza zoezi la kumsajili beki huyo baada ya makubaliano baina yao na villareal kufikia kwenye dau hilo.

Bailly alisajiliwa na Villareal akitokea Espanyol kwa dau la euro 5 milioni 2015 January baada ya Villareal kumuuza beki wao kati Gabriel Paulista kuelekea Arsenal.

Comments