Conte aanza na kipigo


Timu ya Chelsea imeanza vibaya kwenye mechi za kujipima nguvu baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya Rapid Vienna.

Chelsea ambayo ipo chini ya kocha Antonio Conte ilicheza chini ya kiwango na wengi wachezaji hakuwa kwenye kiwango bora hali iliyopelekea kupoteza mchezo huo.

Hata hivyo kocha wa Chelsea Antonio Conte alisema kuwa kwa sasa wamejifunza kutokana na makosa yaliyofanyika kwenye mchezo huo hivyo wanategemea kujipanga zaidi.

"Nadhani tumejifunza kutokana na makosa na makosa, tunategemea kufanya vizuri na kuimarisha mapungufu yetu." Alisema Conte

Comments