Klopp: huu ndio mpango mpya

Baada ya kusaini mkataba mpya na Liverpool jurgen Klopp yupo kwenye mpango mzito wa kuandaa Academy mpya.

Klopp alisaini mkataba wa miaka 6 utakaomuweka Liverpool hadi 2022 na sasa anataka kuifanya timu hiyo kuwa zao la vipaji  barani Ulaya.

"Tunahitaji kuimarisha klabu, tunahitaji timu yetu iendelee zaidi na isonge mbele hayo ndiyo malengo yetu" Alisema Klopp katika mahojiano na Sky sports

Klopp anahitaji kuona timu hiyo inatoa vipaji kama ilivyokuwa kwa Steven Gerrard, Jamie Carragher na  Michael Owen

Comments