Muro aipiga kijembe TFF


Ikiwa ni siku chache baada ya kufungiwa na TFF afisa habari wa Timu ya Yanga Jerry Cornel Muro amepata shavu jipya Ikulu.

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli amemteua Geryson Msigwa kuwa mkurugenzi wa idara ya mawasiliano ikulu na kumteua Jerry Muro kuwa msaidizi wake kwenye idara hiyo.

Jerry Muro ameipiga kijembe TFF baada ya kuandika maneno haya kwenye ukarasa wake wa  Twitter: "Adui yako akikufungia mlango wa sebuleni basi Mungu anakufungulia ule wa uani." Alihitimisha hivyo.

Comments