City ya Gurdiola ni balaa, Ihenacho, Sterling waendelea kutikisa nyavu


Timu ya Manchester city inazidi kuonesha ubora wake EPL baada ya kupata ushindi wa tano mfululizo kwenye ligi hiyo.

Man city imeshinda bao 4-0 katika uwanja wa Etihad, katika mechi hiyo De Bruyne alifunga bao la kwanza, Kelechi Ihenacho alifunga bao la pili, Sterling alifunga bao la 3 na lile la mwisho liliwekwa nyavuni na Ilkay Gundon.

Ushindi huu ni wa nane mfululizo kwa Manchester city ambayo haijapoteza mechi yoyote hadi sasa, ikiwa imeshinda mechi 3 kwenye ligi ya mabingwa Ulaya na mechi 5 kwenye ligi ya EPL.

Comments