Mazembe atwaa ubingwa kombe la Shirikisho barani Afrika


Mabingwa wa Congo DRC TP Mazembe jana wametwaa ubingwa wa kombe la Shirikisho baada ya kuichapa Mo Bejaia jumla ya mabao 5-2.

Jana kwenye uwanja wa nyumbani jiijini Lubumbashi TP Mazembe iliweza kuibuka na ushindi wa bao 4-1 na kunyanyua kombe hilo.

Awali TP Mazembe ilipata sare katika mchezo uliofanyika Algeria kwenye uwanja wa MO Bejaia ambapo timu hizo zilitoka 1-1.

Huu ubingwa wa kwanza kwa TP Mazembe kwenye kombe hilo licha ya kutwaa taji la klabu bingwa Afrika mara tano.

Comments