Tetesi: nyota wa Chelsea kutua Inter


Timu ya Intermilan bado haijaachana na mpango wa  kuinasa saini ya kiungo mshambuliji  wa Chelsea Oscar.

Oscar ameshindwa kupata nafasi katika timu ya kwanza ya kocha Antonio Conte tangu alipoanza kutumia mfumo wa 3-4-3 baada ya kuyumba katika mechi za awali.

Huenda nyota akatimka Serie A mwezi January baada ya Conte kuweka wazi kuwa atampiga bei Mbrazil huyo endapo atapokea ofa ya kutosha.

mbali na Oscar huenda Cesc Fabrigas akatimka Serie A baada ya AC Milan na Juventus kuonesha nia ya dhati kumsajili mhispania huyo.

Comments