Man utd yatinga 16 bora Europa ligi, yashinda ugenini


Timu ya Manchester united imefanikiwa kutinga hatua ya 16 bora baada ya kuitwanga St Etienne jumla ya mabao 4-0.

Katika mchezo wa kwanza Man utd ikiwa nyumbani iliilaza St Etienne kwa bao 3-0 kwa sifuri bao zote zikiwekwa nyavuni na Ibrahimovic.

Man utd imefunga hesabu ya goli 4-0 baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa marudiano uliopigwa nchini Ufaransa.

Bao la pekee la ushindi la Man utd lilifungwa na Kiungo Henrink Mkhitaryan katika dakika ya 17 ya mechi hiyo.

Comments