Timu ya Real Madrid imeshindwa kufurukuta mbele ya Las Palmas baada ya kutoka sare ya bao 3-3 katika uwanja wa Santiago Bernabeu.
Real Madrid ilipata bao la kuongoza kupitia Isco aliyefunga dakika ya 8 hata hivyo kiungo wa Las Palmas Tana alichomoa bao dakika ya 10.
Kipindi cha pili Las Palmas walipata bao na kuyafanya matokeo kuwa 3-1, lakini Christiano Ronaldo alichomoa bao hizo na matokeo kuwa 3-3.
Pia katika mchezo huo mshambuliaji wa kimataifa wa Wales Gareth Bale alitolewa nje ya uwanja baada ya kuoneshwa kadi nyekundu na mwamuzi katika dakika ya 47 ya mechi hiyo.

Comments
Post a Comment