Mabingwa wa kombe la Mapinduzi Azam FC wamefanikiwa kutinga nusu fainali ya kombe la shirikisho baada ya kuitwanga Ndanda bao 3-1 katika uwanja wa Chamanzi Complex.
Mshambuliaji kinda ambaye anachipukia kwenye kikosi cha Azam kwa sasa Shaban Idd alifunga mabao 2, na lingine la 3 likiwekwa nyavuni na Ramadhan Singano 'Messi'.
Azam imeungana na Simba pamoja na Mbao ambazo zilishatinga nusu fainali na sasa wanasubiri matokeo kati ya Yanga na Prisons ambao watacheza kesho.

Comments
Post a Comment