Man city imekamilisha usajili wa kwanza.

May 26, 2017

Manchester City ipo mbioni kukamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji kutoka Monaco Bernardo Silva kwa dau la £43 milioni.

Bernardo Silva atasaini miaka mitano na kujiunga na rasmi na Manchester City ifikapo June 1 mwaka huu dirisha hilo la usajili litakapokuwa limefunguliwa.

Huo ni usajili wa kwanza uliofanywa na Man city kuelekea dirisha kubwa la usajili ambapo bado wako mbioni kusaka nyota wakali zaidi.

Comments