Mei 6, 2017
Timu ya West Ham United imepunguza kasi ya Tottenham kwenye mbio za ubingwa wa ligi kuu baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 katika uwanja wa Olympic.
Bao pekee la West Ham United lilifungwa katika dakika ya 65 ya mchezo na kiungo machachali Manuel Lanzini.
Spurs itakuwa imetengeneza pengo la pointi 7 endapo Chelsea itashinda dhidi ya West Brom wikiendi hii na kuendelea ikiwa ni hatua nzuri katika mbio za ubingwa.

Comments
Post a Comment